Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 94 2023-04-17

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI K.n.y. MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: -

Je, lini barabara ya Kibaoni – Endala – Endamarik hadi Endabash itajengwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Awack Tlemai, Mbunge wa Jimbo la Karatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza matengenezo katika barabara ya Kibaoni – Endala - Endamariek hadi Endabash. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilipeleka shilingi milioni 599.97 kwa ajili ya ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 40 kwenye barabara hiyo, na ujenzi wake umekamilika. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Serikali imetenga shilingi milioni 68 kwa ajili ya matengenezo ya sehemu korofi yenye urefu wa kilomita tano katika barabara hiyo na utekelezaji wake unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali itatenga shilingi milioni 213.02 kwa ajili ya kujenga madaraja mawili katika matengenezo ya sehemu korofi yenye urefu wa kilometa 10 pamoja na matengenezo ya muda maalum yenye urefu wa kilomita mbili katika barabara hiyo.