Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 8 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 96 2023-04-17

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA: aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutimiza masharti ya ajira kwa Watumishi ikiwemo kuwapandisha madaraja na stahiki zingine?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutekeleza matakwa ya kisera, kisheria na miongozo mbalimbali ya kiutawala na kiutumishi inayolenga au inayoelekeza Serikali katika kumtimizia masharti na haki za mtumishi wake. Aidha katika kufanya hivyo Serikali imeendelea na Utaratibu wa kupandisha madaraja watumishi ikiwemo utaratibu wa mpandisho wa mserereko. Pamoja na hilo Serikali imeendelea pia kuongeza kima cha chini cha mshahara na pia kuongeza allowance katika kazi za ziada na posho za muda wa ziada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hilo pia mwaka 2021/2022, Serikali ililipa shilingi bilioni 124.3 kwa watumishi 75,007 ikiwa ni malimbikizo (arrears) ya mishahara. Vilevile, Serikali iliongeza umri wa watoto wa watumishi wa umma kunufaika na huduma ya bima kutoka miaka 18 hadi miaka 21 ambapo katika kipindi cha mwaka mmoja jumla ya watoto 65,353 wamesajiliwa.