Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 110 2023-04-18

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa soko la Kimataifa la Ndizi katika Kata ya Kiwira utaanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Jimbo la Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Soko la Kisasa la Ndizi, Kiwira, katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe imeanza maandalizi ya kutekeleza mradi huo kwa kufanya Upembuzi yakinifu, kuandaa michoro ya kihandisi, kupima udongo wa eneo la ujenzi na kuandaa andiko la kuomba fedha kwa ajili ya mradi huo.

Mheshimiwa Spika, andiko limewasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango kwa uchambuzi na pindi litakapopitishwa, mradi utatengewa fedha za ujenzi kupitia utaratibu wa miradi ya kimkakati. Ahsante.