Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 114 2023-04-18

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA K.n.y. MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, Mbunge wa Solwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige yenye urefu wa kilometa 148.8 kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Jumla ya kilometa 5.65 za sehemu ya Kahama kwenye barabara hii zimejengwa kwa kiwango cha lami na mita 540, sehemu ya Bulige imejengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, aidha, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali imetenga shilingi milioni 750.62 kwa ajili ya ujenzi wa kilometa 1.2, sehemu ya Solwa na Bulige ambapo mkandarasi tayari amepatikana na ameshakabidhiwa mradi ili kuanza kazi. Ujenzi umepangwa kukamilika mwezi Septemba, 2023, ahsante.