Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 9 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 117 2023-04-18

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka katazo la kisheria la kuswaga mifugo ili kuzuia uharibifu wa mazingira?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, usafirishaji wa mifugo hufanyika chini ya Sheria ya Magonjwa ya Wanyama, Sura 156 na Kanuni zake za Udhibiti wa Usafirishaji wa Wanyama na Mazao ya Wanyama, G.N. 28 za mwaka 2007, ambapo usafirishaji wa mifugo kutoka wilaya moja kwenda nyingine hufanyika baada ya mifugo kukaguliwa na wataalam na kupatiwa kibali cha kusafirishwa. Aidha, Waraka wa Rais Na.1 wa Mwaka 2002 uliziagiza Serikali za Mitaa kote nchini kutunga sheria ndogo ili kuzuia uswagaji wa mifugo.

Mheshimiwa Spika, kwa maelezo hayo hapo juu inathibitisha kwamba sheria ipo. Hivyo basi, wafugaji wanahimizwa kuzingatia Sheria ya Magonjwa ya Wanyama, Sura 156 pamoja na sheria ndogo zilizopo ndani ya halmashauri zao zinazozuia uswagaji wa mifugo. Pia, nitumie fursa hii kuzielekeza halmashauri ambazo mpaka sasa hazijatunga sheria ndogo za kuzuia uswagaji wa mifugo zifanye hivyo mara moja.