Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 10 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 129 2023-04-19

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: -

Je, ni wananchi wangapi wa Jimbo la Nanyumbu wamefidiwa kutokana na uharibifu uliofanywa na tembo katika mashamba yao?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka 2022/2023, Wizara ilipokea jumla ya maombi nane kutoka kwa wananchi wa Vijiji vya Mchenjeuka, Lukula, Masuguru, Marumba na Mpombe walioathiriwa na matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu katika Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu. Baada ya taratibu za malipo kukamilika, mnamo tarehe 21 Machi, 2023, Wizara ilifanya malipo ya kifuta jasho ya jumla ya shilingi 5,160,000 kwa wananchi saba wa Vijiji vya Michenjeuka, Lukula, Masuguru na Mpombe walioharibiwa mazao. Aidha, mwezi Machi mwaka huu, Wizara ilipokea maombi mapya 12 ya wananchi wa Vijiji vya Nanyumbu na Marumba ambayo yanaendelea kushughulikiwa kwa ajili ya kuandaa malipo.