Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 136 2023-04-20

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga barabara ya Kwamtoro - Sanzawa hadi Mpendo katika Wilaya ya Chemba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya marekebisho ya kipande cha Sanzawa – Mpendo chenye urefu wa kilomita 38.2 ambapo shilingi bilioni 2.06 zinahitajika. Serikali imeendelea kuihudumia barabara hiyo ambapo mwaka wa fedha wa 2022/2023 shilingi milioni 48 zimepelekwa kwa ajili ya kufanya matengenezo kwenye maeneo korofi yenye urefu wa kilomita Nane kati ya Kwamtoro na Sanzawa katika Vijiji vya Kurio na Moto. Aidha, ukarabati wa box culvert katika Kijiji cha Moto umekamilika. Kwa sasa Mkandarasi anafanya maandalizi ya kuchonga barabara eneo korofi la Kurio lenye urefu wa kilomita Tatu.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2023/2024, serikali itatenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya kuanza kufanya matengenezo kwenye eneo korofi la mawe kati ya Sanzawa na Mpendo lenye urefu wa kilometa 34.2.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara za Jimbo la Chemba kulingana na upatikanaji wa fedha ili kuimarisha usafiri na usafirishaji.