Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 11 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 137 2023-04-20

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, kwa nini wanufaika wa TASAF wasilipwe mkononi badala ya kupewa kwa njia ya simu na benki?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu Swali lililoulizwa na Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwaka 2019 Serikali ilifanya majaribio ya mfumo wa kieletroniki wa malipo kwa walengwa katika mamlaka za utekelezaji 19. Baada ya majaribio, mwaka 2020 mfumo wa malipo kwa njia ya kielektroniki ulipitishwa rasmi na walengwa kuanza kutumia mfumo huo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inakiri kutokea changamoto katika baadhi ya maeneo ya utekelezaji. Hivyo utaratibu wa malipo kwa sasa upo katika njia tatu; kwa njia ya simu, akaunti ya benki na njia ya malipo ya fedha taslimu.

Mheshimiwa Spika, kwa msingi huu ni uchaguzi wa mnufaika mwenyewe atumie njia gani kadri ya mazingira yake. Aidha, naomba kutoa rai kwa Mheshimiwa Mbunge tusaidiane kuelimisha walengwa juu ya njia hizi kuu tatu za malipo.