Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 11 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 139 2023-04-20

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Iyari hadi Mkunwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania imepanga kujenga kilometa 2.2 katika barabara ya Iyari – Mkunwa (kilometa 79) kwa kiwango cha lami na mkandarasi yupo anaendelea na ujenzi ambapo kazi zinatarajiwa kukamilika Juni, 2023. Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha hadi kuikamilisha yote, ahsante.