Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 11 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 142 2023-04-20

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza: -

Je, ni lini umeme wa REA utafika katika Kijiji cha Ikombe – Kyela?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Kyela, kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Ikombe kitapata huduma ya umeme kupitia Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaotekelezwa na Mkandarasi M/s ETDCO Ltd. Kazi ya ujenzi wa miundombinu ya umeme katika Kijiji cha Ikombe kutoka Kijiji cha Lyulilo inatarajiwa kuanza mwezi Mei, 2023 na inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.