Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 147 2023-04-24

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Watu Wenye Ulemavu mitaji katika Jimbo la Mbogwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nicodemas Henry Maganga, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ilitenga shilingi milioni 56 kwa ajili ya mikopo ya watu wenye ulemavu. Hadi kufikia mwezi marchi, 2023 jumla ya vikundi 6 vya watu wenye ulemavu vimekopeshwa kiasi cha shilingi milioni 34. Fedha hizi zimewezesha vikundi vya watu wenye ulemavu kuanzisha biashara na kujiongezea kipato.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe imetenga shilingi milioni 56.19 kwa ajili ya mikopo isio na riba kwa vikundi vya watu wenye ulemavu. Fedha hizi zitatolewa kupitia mfumo ulioboreshwa wa asilimia 10, ahsante.