Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 153 2023-04-24

Name

Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE K.n.y MHE. TOUFIQ S. TURKY aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa Saratani nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taufiq Salim Turky, Mbunge wa Mpendae, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitumia njia mbalimbali za kutoa elimu kwa umma kuhusu kujikinga na ugonjwa wa saratani kupitia vipindi vya redio na televisheni, machapisho na magazeti, mitandao ya jamii kama Facebook, Instagram na pia televisheni sehemu za kusubiria wagonjwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ya kutoa elimu ya ugonjwa wa saratani kama ifuatavyo: -

(i) Kuandaa kampeni mbalimbali za uelimishaji wa jamii na uchunguzi wa awali wa saratani nchini ikiwemo huduma Mkoba.

(ii) Kuandaa mtaala wa mafunzo wa magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo saratani kwa watoa huduma wa ngazi za msingi ili kuwajengea uwezo wa kutoa elimu kwa jamii.

(iii) Kuandaa vipindi mbalimbali na machapisho ya utoaji wa elimu ya afya dhidi ya magonjwa yasisyo ya kuambukiza ikiwemo saratani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.