Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 154 2023-04-24

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Meli ndogo ya abiria Muleba pamoja na kutumia meli ya MV Victoria kujaribu masoko ya nchi za Uganda na Kenya?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa ujenzi na uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles John Mwijage, Mbunge wa Muleba Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua hitaji kubwa la usafiri wa wananchi Wilayani Muleba hususani waishio katika Visiwa. Kwa kutambua hitaji hilo, Serikali kupitia Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) imetenga meli moja iitwayo MV Clarias kutoa huduma katika Visiwa vya Godziba Wilayani Muleba na Visiwa vya Gana Wilayani Ukerewe. Meli hiyo iliyokuwa imeanza kutoa huduma katika visiwa hivyo tarehe 3 Machi, 2023 ilisimama tarehe 22 Machi, 2023 baada ya kupata hitilafu za kiufundi. Huduma hizo zitaendelea kuanza tena mwanzoni mwa mwezi Mei, 2023 baada ya matengenezo kukamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu huduma za safari za kwenda Uganda na Kenya, MSCL inatarajia kuanza safari hizo kwa kutumia meli ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu mara baada ya ujenzi wake kukamilika. Meli ya MV Victoria haitaweza kutumika kwani ndiyo meli pekee inayotegemewa katika utoaji wa huduma za usafiri kati ya Mwanza na Bukoba kupitia Kemondo na ni msaada mkubwa kwa wakazi wa ukanda huo. Ahsante. (Makofi)