Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 1 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 9 2016-09-06

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA (K.n.y. MHE. SAADA MKUYA SALUM) aliuliza:-
Vituo vingi vya afya vya kijeshi vinahudumia maafisa wa jeshi na wananchi waliopo karibu na vituo hivyo. Hata hivyo vituo hivi vinakabiliwa na upungufu wa dawa, vifaa tiba na wataalam wenye ujuzi.
(a) Je, Serikali inafahamu idadi ya vituo vyake vilivyopo Zanzibar?
(b) Je, kuna mkakati gani unafanyika kuhakikisha kuwa vituo hivyo vinapatiwa dawa, vifaa tiba na wataalam wa kuhudumia wananchi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saada Mkuya Salum Mbunge wa Weleza kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, kulingana na vipimo vya Umoja wa Mataifa (United Nations – UN), Zanzibar ina kituo kimoja cha afya ngazi ya tatu na vituo viwili ngazi ya pili. Aidha kimuundo kila Kikosi cha Jeshi kina kituo kidogo cha tiba.
(b) Kwa ujumla vituo vya afya vina changamoto za dawa, vifaa tiba na wataalam. Hali hiyo kwa kiasi kikubwa inachangiwa na ufinyu wa bajeti. Hata hivyo, changamoto hizo kwa sehemu kubwa zinategemewa kutatuliwa baada ya kukamilika taratibu za kuanzishwa mfuko wa Bima ya Afya kwa jeshi letu.
Aidha, changamoto ya wataalamu wa afya inategemewa kupungua baada ya wataalam wa afya walioajiriwa hivi karibuni waliopo katika mafunzo ya vitendo vikosini (exposure) na kwenye Vyuo vya Kijeshi kuhitimu mafunzo yao. Pia, upo mpango wa kuandikisha wataalamu wa afya katika ngazi ya Paramedics baada ya kupata kibali cha ajira mpya. Pia upo mpango wa kuandikisha wataalam wa afya katika ngazi Paramedics mara tu baada ya ajira mpya kuruhusiwa.