Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 11 2016-09-06

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:-
Ni muda mrefu sasa Kikosi cha Polisi Marine Pemba hakina boti ya doria hali inayopelekea polisi kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
(a) Je, Serikali inatambua hilo?
(b) Kama inalitambua, je, ni lini Serikali itakipatia Kikosi cha Polisi Marine Pemba boti za doria ili kuwawezesha polisi hao kufanya kazi zao kwa ufanisi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Kombo Hamad, Mbunge wa Wingwi, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inalitambua tatizo la Polisi Wanamaji Pemba kukosa boti ya doria. Serikali itawapatia Polisi Wanamaji Pemba boti pale uwezo wa kibajeti utakapoongezeka kwani boti zilizopo haziwezi kuhimili mkondo wa maji uliopo Nungwi kuelekea Pemba.