Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 214 2023-05-03

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: -

Je, lini Shule za Sekondari za Lyamahoro na Rubale zitaanza kutoa elimu ya kidato cha tano na sita?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na jitihada za kuongeza shule za kidato cha tano na sita katika halmashauri zote nchini kwa kuongeza miundombinu ya mabweni, madarasa na bwalo. Kupitia jitihada hizo, Shule ya Sekondari Lyamahoro imepata sifa ya kuwa Shule ya Kidato cha Tano na Sita na inatarajia kuanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha tano kwa Mchepuo wa CBG Julai, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Sekondari Rubale bado haina miundombinu ya kutosha kuiwezesha kuwa ya kidato cha tano na sita. Nitumie nafasi hii kumuomba Mheshimiwa Mbunge kushirikiana na wananchi kuanza kujenga miundombinu mingine na Serikali itatekeleza kulingana na upatikanaji wa fedha.