Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 215 2023-05-03

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari ya Rubanga ili iwe ya kidato cha tano na sita?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Jimbo la Geita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuwezesha shule za sekondari kuwa za kidato cha tano na sita ikiwemo upelekaji wa walimu wenye sifa na taaluma stahiki, ujenzi wa miundombinu ya mabweni na madarasa pamoja na upelekaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Kuanzisha shule ya kidato cha tano na sita kunategemea pia eneo, pamoja na uhitaji kulingana na wingi wa wanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepokea ombi la Mheshimiwa Mbunge na itatekeleza kulingana na uhitaji na upatikanaji wa fedha. Aidha, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita tayari ina shule tatu za kidato cha tano na sita za Kamena, Butundwe na Bugando, naomba kuchukua fursa hii kumshauri Mheshimiwa Mbunge tuimarishe shule za kidato cha tano na sita zilizopo ili kuendelea kupokea wanafunzi kulingana na uhitaji kwa sasa.