Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 216 2023-05-03

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: -

Je, ni kero zipi za Muungano zilizoibuliwa na kutatuliwa toka kuasisiwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khalifa Mohamed Issa Mbunge wa Mtambwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali za pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zimejadili na kuzipatia ufumbuzi jumla ya changamoto 22, ambapo baadhi ya

changamoto hizo ni gharama za kushusha mizigo Bandari ya Dar es Salaam kwa mizigo inayotoka Zanzibar, utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia, utaratibu wa vikao vya kamati za pamoja za SJMT na SMZ vya kushughulikia masuala ya Muungano. Aidha, changamoto zote zilizopatiwa ufumbuzi zimefafanuliwa kwa kina na zinapatikana kupitia tovuti yetu ya Ofisi ya Makamu wa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja zilizobakia kutatuliwa ni nne, ambazo ni Mapendekezo ya Tume ya Pamoja ya Fedha, Usajili wa Vyombo vya Moto, Uingizaji wa Sukari katika Soko la Tanzania Bara, na Mgawanyo wa Mapato Yatokanayo na Hisa za SMZ zilizokuwa katika Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki na Faida ya Benki Kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.