Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 217 2023-05-03

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Vituo vya Abiria vya Bugorola, Ukara na Kisorya Ukerewe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) katika mwaka wa fedha 2022/2023, umetenga fedha kiasi cha shilingi 332,220,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Abiria vya Bugorola, Ukara na Kisorya katika Wilaya ya Ukerewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TEMESA imeingia makubaliano na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA - Mwanza) kwa ajili ya kufanya usanifu wa miundombinu ya majengo na mchanganuo wa makadirio ya gharama husika. Taratibu za kumpata Mkandarasi atakayejenga miundombinu hiyo zitatekelezwa baada ya usanifu kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha 2022/2023, ahsante.