Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 220 2023-05-03

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza ajali zinazosababishwa na magari ya mchanga Wilaya ya Kaskazini B - Unguja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la Kaskazini A na B – Unguja ajali zilizotokea kuanzia Januari, 2021 hadi Desemba, 2021 ni tatu ambazo zimesababisha vifo vya watu wanne na majeruhi mmoja. Ajali zilizotokea kuanzia Januari, 2022 hadi Machi, 2023 ni moja na imesababisha kifo cha mtu mmoja. Kwa jumla kesi zilizofikishwa mahakamani ni nne na zilizopata hukumu ni tatu na kesi moja inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajali zinazosababishwa na magari ya kubeba mchanga zimeendelea kupungua kutokana na Serikali kuweka alama za matumizi ya barabara, kuweka Kituo cha Ukaguzi wa Magari, kukagua leseni za madereva, kuweka utaratibu wa kupima macho na kutoa elimu ya matumizi bora na sahihi ya barabara kwa watumiaji wote, nashukuru.