Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 222 2023-05-03

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kushusha bei ya mbolea na pembejeo nyingine za kilimo ili kuongeza uzalishaji?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa niaba ya Waziri wa Kilimo ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ya kupunguza gharama za upatikanaji wa mbolea na pembejeo nyingine kwa wakulima ili kuongeza uzalishaji na tija kwa mazao ya kilimo. Mikakati hiyo ni pamoja na kutoa ruzuku ya mbolea, mbegu bora kwa mazao ya alizeti, miche ya chikichi, parachichi, chai na kahawa pamoja na viuatilifu vya mazao ya korosho, pamba na viuatilifu kwa ajili ya kudhibiti milipuko ya visumbufu vya mimea ikiwemo viwavijeshi, inzi, panya, kweleakwelea na nzige.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia Aprili, 2023 jumla ya tani 349,922 za mbolea zimenunuliwa na wakulima 799,937 kwa bei ya ruzuku. Vilevile, Serikali imetoa jumla ya lita 48,033 za viuatilifu vya kudhibiti viwavijeshi, ekapaki 1,823,688 za viuatilifu vya pamba, tani 15,015.03 na lita 2,684,470.5 za viuatilifu vya zao la korosho, tani 1,004 za mbegu bora za alizeti na miche bora 61,486,981 ya mazao mbalimbali kwa utaratibu wa ruzuku. Aidha, utaratibu wa utoaji wa ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa wakulima utaendelea kufanyika kulingana na bajeti ya Serikali. (Makofi)