Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 223 2023-05-03

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawalipa fedha zao waathirika wa Benki ya FBME iliyofilisiwa tangu Mei, 2017?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, na kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haji Makame Mlenge, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi mwezi Machi, 2023, Serikali kupitia Bodi ya Bima ya Amana - DIB imelipa jumla ya shilingi bilioni 2.43 kama malipo ya awali ya fidia ya Bima ya Amana kwa wateja 3,446 waliojitokeza wa Benki ya FBME iliyofilisiwa mnamo mwezi Mei, 2017. Malipo ya fedha za ufilisi (liquidation proceeds) kwa wateja wenye amana zaidi ya shilingi 1,500,000 yanayotokana na uuzaji wa mali, makusanyo ya madeni na fedha nyingine za Benki ya FBME yatafanyika baada ya Mahakama ya Cyprus kutoa uamuzi kuhusu pingamizi lililowekwa na Benki Kuu ya Cyprus la kuitambua DIB kama Mfilisi wa benki yote ikijumuisha Makao Makuu pamoja na tawi la Cyprus.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, uamuzi wa Mahakama unatarajiwa kutolewa ndani ya mwaka huu wa fedha 2022/2023, ahsante.