Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 224 2023-05-03

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isiagize kuwe na madereva na kondakta wa jinsia zote kwenye mabasi ya shule ili kudhibiti vitendo vya ubakaji?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Waraka wa Elimu Na. 1 wa Mwaka 2023 imetoa maelekezo kwa wamiliki wote wa shule zinazotoa huduma ya usafiri kwa wanafunzi kuhakikisha kuwa wanakuwa na mhudumu wa kike na wa kiume katika kila basi au gari linalosafirisha wanafunzi kuanzia mwanzo hadi mwisho wa safari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Waraka huo, Wizara ilikutana na wadau wa elimu kujadiliana namna bora ya kutekeleza Waraka tajwa na tulikubaliana kwamba deadline ya kutekelezwa imefutwa. Hivyo, wadau wote wanatakiwa kujitahidi kutekeleza Waraka huo na kabla ya kupanga deadline nyingine tutapanga kikao na wadau wote kujadiliana namna ya utekelezaji. Kwa sasa tunahimiza kwamba, mabasi yote ya wanafunzi yawe na watumishi au wahudumu wa jinsia zote. Ninakushukuru sana.