Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 17 Water and Irrigation Wizara ya Maji 225 2023-05-03

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Maruku, Karabagaine, Nyakato, Kunazi, Katoma, Kemondo na Bujugo Jirani na Bukoba Manispaa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa maji Kata ya Katoma na wananchi wanapata huduma ya maji. Vilevile, utekelezaji wa miradi ya maji unaendelea kwenye Kata za karabagaine na Nyakato ambapo miradi imekamilika katika vijiji vya Itahwa, Kabale na Burugo. Maeneo ya Kemondo na Kunazi utekelezaji wa mradi unaendelea na umefikia asilimia 88. Kwa Kata za Maruku na Bujugo, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kumuajiri Mkandarasi na ujenzi utaanza mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi kwenye vijiji vilivyobaki katika Kata za Karabagaine na Nyakato.