Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 252 2023-05-08

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kukomesha vifo na upotevu wa mali kutokana na migogoro ya wakulima na wafugaji katika Wilaya ya Kilwa, Nachingwea na Liwale?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoani Lindi ni miongoni mwa Mikoa ambayo imekuwa na ongezeko kubwa la wafugaji wanaohamia na mifugo yao ikiwemo ng’ombe na mbuzi katika kipindi miaka ya karibuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Lindi umekumbwa na migogoro ya wakulima na wafugaji katika Wilaya za Kilwa, Liwale na Nachingwea. Migogoro hii imesababishwa na ongezeko la mifugo iliyopelekea kuongezeka kwa mahitaji ya malisho na maji, ukosefu wa mipango ya matumizi ya ardhi, uuzaji holela wa ardhi na wakulima kuvamia maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ufugaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha inaondoa changamoto ya migogoro ya aridhi kwa kutekeleza yafuatayo: - kutenga maeneo kwa ajili ya mifugo, ujenzi wa miundombinu ya mifugo, kuwezesha upatikanaji wa malisho, uanzishwaji wa ranchi ndogo ndogo, kuweka utaratibu wa uingizwaji wa mifugo katika Mkoa wa Lindi, kuunda kamati za usuluhishi wa migogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatoa kwa viongozi ngazi ya Mkoa na Halmashauri kote nchini kuhakikisha wanatatua migogoro kwa wakati, hii ikiwa pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa matumizi ya ardhi.