Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 254 2023-05-08

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhimiza vijana kushiriki shughuli za kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, azma ya Serikali na Ilani ya Chama cha Mapinduzi ni kutengeneza ajira milioni nane kwa vijana ifikapo mwaka 2025 ili kutatua changamoto ya ajira kwa vijana. Hatua ya awali ambayo imechukuliwa na Serikali pamoja na mambo mengine ni kufanya tathmini na kutambua sababu kubwa inayofanya vijana wasipende kujishughulisha na kilimo, ambapo imeonekana kuwa kukosekana kwa ardhi, mitaji, miundombinu ya umwagiliaji na masoko ya uhakika ni sababu kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza kuweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha inatatua changamoto hizo na kuvutia vijana kushiriki katika kilimo. Moja ya mkakati huo ni Mradi wa Jenga Kesho iliyo Bora (Building a Better Tomorrow) ambapo Serikali imetenga maeneo ya kilimo na kuwamilikisha vijana, inaweka miundombinu ya umwagiliaji, inawawezesha kupata mitaji na masoko ili wanufaike na shughuli za kilimo.