Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Energy and Minerals Wizara ya Madini 260 2023-05-08

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti katika maeneo yanayoonekana kuwa na madini ili wananchi wanufaike?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI K.n.y. WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini nijibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Kainja Andrea, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) inaandaa mpango wa kufanya utafiti kwenye maeneo yanayoonekana kuwa na viashiria vya madini ikiwemo madini ya kimkakati. GST imepewa mamlaka ya kisheria kufanya utafiti wa madini nchini kwa lengo la kupata taarifa za kina za uwepo wa madini katika maeneo husika. Wizara ya Madini imeshaielekeza GST kuandaa mpango wa utafiti wa madini wa nchi kwenye maeneo ya kipaumbele ili kuombea bajeti ya kufanya kazi hiyo. Nashukuru.