Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 20 Water and Irrigation Wizara ya Maji 262 2023-05-08

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatatua changamoto ya maji katika Kata za Mkalamo, Magamba Kwalukonge na Mkomazi Wilayani Korogwe?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua adha ya maji inayowakabili wananchi wa Kata za Mkalamo, Magamba, Kwalukonge na Mkomazi Wilayani Korogwe. Hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa kukabiliana na hali hiyo na katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imechimba visima viwili virefu, kufunga pampu na kujenga tenki la lita 75,000 ambapo wananchi wa vijiji vya Magamba, Kwalukonge, Changalikwa na Makole Kata ya Magamba Kwalukonge wanapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kwa Kata zilizobaki, Serikali itajenga miradi ya maji kupitia chanzo cha Mto Pangani, Mtaalam ameajiriwa na anaanza kazi mwezi Mei, 2023 na utekelezaji wa miradi utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024.