Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 309 2023-05-12

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: -

Je, lini Daraja la Lyusa na Itembe na kalavati la Nkoma, Lyusa na Mwanjolo vitajengwa ili Daraja la Sibiti lipitike mwaka mzima?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, daraja la Lyusa na makalavati ya Nkoma, Lyusa na Mwanjolo yamejumuishwa katika mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa yenye urefu wa kilometa 389 ambapo Mkandarasi ameshapatikana na mkataba wa ujenzi unatarajiwa kuwa umesainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa daraja la Itembe lenye urefu wa mita 150 lililopo katika Mkoa wa Simiyu, kazi za ujenzi zinaendelea na zimepangwa kukamilika mwezi Oktoba, 2023; ahsante.