Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 310 2023-05-12

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, lini Mradi wa Bwawa la kufua umeme wa RUSUMO utazinduliwa ili kuondoa tatizo la kukatika kwa umeme Ngara?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swala la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa kufua umeme wa Rusumo wa Megawati 80 wa nchi tatu za Tanzania, Burundi na Rwanda ambazo zitagawanywa sawa, umefikia asilimia 99 na utaanza kufanya kazi mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, mashine tatu za kuzalisha umeme zitawashwa kwa mashine moja kila mwezi kuanzia mwezi wa Juni na hivyo tunatarajia kuuzindua baada ya mwezi wa saba baada ya kuwashwa kwa mashine zote tatu kukamilika, nashukuru.