Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 363 2023-05-18

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, lini shule za Sekondari Nyamtukuza, Muhange, Shuhudia, Kasanda na Gwanumpu zitakuwa za kidato cha tano na kidato cha sita?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari ya Muhange imekaguliwa na wadhibiti ubora wa shule ikaonekana ina mapungufu ya mabweni mawili, mapungufu hayo yakikamilishwa itapandishwa hadhi ya kuwa kidato cha tano na sita.

Mheshimiwa Spika, Shule za Nyamtukuza, Shuhidia, Kasanda na Gwanumpu zinaendelea kuongezewa miundombinu ya majengo, ikikamilika zitakaguliwa na wadhibiti ubora wa shule na kuombewa kupandishwa kuwa za Kidato cha Tano na Sita. Hata hivyo, shule moja mpya ya kidato cha tano na sita imesajiliwa ambayo inaitwa Amani Mtendeni.