Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 365 2023-05-18

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: -

Je, kiasi gani cha bajeti kimetengwa TARURA miaka mitatu mfululizo kwa ajili ya ukarabati wa barabara Kyerwa na upi ufanisi wake?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka wa fedha wa 2020/2021 hadi 2022/2023, Wilaya ya Kyerwa imetengewa jumla ya shilingi bilioni 7.34, ambapo mwaka 2020/2021 shilingi bilioni 1.26 zilitengewa, mwaka 2021/2022 shilingi bilioni 2.89 na shilingi bilioni 3.18 zimetengwa katika mwaka wa fedha wa 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, ufanisi uliopatikana ni kuwa, barabara zenye kiwango cha changarawe zimeongezeka kutoka kilomita
185.46 hadi kilometa 261.71 na barabara za udongo kupungua kutoka kilomita 711.96 hadi kilometa 634.81 na makalvati 95 yamejengwa, ikiwa ni pamoja na barabara za lami zenye urefu wa kilometa 4.2 katika Makao Makuu ya Wilaya na Mji Mdogo wa Biashara wa Nkwenda.