Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 366 2023-05-18

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza: -

Je, kwa kiasi gani ushiriki wa Tanzania katika mikutano ya Kimataifa unazingatia upatikanaji wa fursa za kiuchumi na utekelezaji wake?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ushiriki wa Tanzania katika mikutano ya Kimataifa unalenga kupata na kutumia fursa za kiuchumi ikiwa ni pamoja na kupata mitaji, uwekezaji, masoko ya bidhaa na huduma, kukuza utalii, miradi ya kisekta, mikopo ya masharti nafuu na misaada, kujengewa uwezo wa kitaalamu na upatikanaji wa teknolojia.

Mheshimiwa Spika, ushiriki wa Tanzania katika mikutano ya Kimataifa umewezesha Tanzania kupata masoko ya bidhaa mbalimbali, kama vile mbogamboga, matunda, korosho, nafaka, utalii, malumalu na bidhaa za kioo. Vilevile nchi yetu inanufaika kwa kupata wawekezaji katika sekta mbalimbali, ikiwa ni pamoja na utalii, viwanda, kilimo, uvuvi, mifugo, madini na nishati anuwai.

Mheshimiwa Spika, kadhalika katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya Sita, ushiriki wa Tanzania katika mikutano ya Kimataifa umeiwezesha Tanzania kupata misaada mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha kutoka Shirika la Fedha Duniani kiasi cha shilingi trilioni 1.3 kwa ajili ya kukabiliana na janga la UVIKO- 19.

Mheshimiwa Spika, Benki ya Dunia kutenga kiasi cha dola za Marekani bilioni 2.1 (sawa na shilingi trilioni 4.8) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka 2023/2024 na 2024/2025, na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kutoa dola za Marekani milioni 58.5 kwa ajili ya miradi ya kilimo kwa mwaka 2021/2022. Aidha, kupitia ushiriki katika Mkutano wa 27 wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi (COP 27), Benki ya Dunia ilizipatia Nchi za Afrika ikiwemo Tanzania, kiasi cha dola za Marekani bilioni 18 kwa ajili ya miradi ya nishati jadidifu, ahsante sana.