Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 367 2023-05-18

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, lini Serikali italeta muswada wa sheria ya adhabu kali kwa wanaobaka na kulawiti watoto na wanawake?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa vifungu 130, 131, 131A na 154 vya Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16, ni makosa ya jinai kwa mtu kubaka na kulawiti. Makosa yote haya adhabu yake ya juu ni kifungo cha maisha jela, na adhabu ya chini ni kifungo cha miaka 30 jela. Aidha, kwa makosa yote hayo yakitendeka dhidi ya mtoto mwenye umri chini ya miaka 10, adhabu yake ni kifungo cha maisha jela. Pamoja na adhabu hizo, Mahakama ina mamlaka ya kutoa amri ya ziada ya kumlipa fidia mwathirika chini ya kifungu cha 131(1) cha Kanuni za adhabu.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali katika kutekeleza maelekezo ya Bunge, inafanya utafiti zaidi ili kuona kama kuna hitaji la kufanya maboresho au marekebisho ya sheria hiyo, ahsante.