Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 368 2023-05-18

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, kwa kiasi gani Taifa linanufaika na vijana wanaopelekwa kwenye mafunzo ya kilimo Israel?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Israel zilikubaliana kushirikiana kwa kuanzisha programu ya kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wanaomaliza Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati vya Mafunzo ya Kilimo na Mifugo nchini Israel. Lengo la programu hiyo ni kuongeza ujuzi na maarifa juu ya teknolojia za kisasa.

Mheshimiwa Spika, kuanzia mwaka 2015 hadi sasa, jumla ya vijana 261 wa Kitanzania wamenufaika na mafunzo ya kilimo kupitia Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Israel (Ministry of Foreign Affairs Israel’s Agency for International Develeopment Cooperation) kupitia Agrostudies.

Mheshimiwa Spika, Wizara imeanza kuwatumia vijana waliohitimu mafunzo kwa vitendo nchini Israel kupitia programu ya BBT na Block farm ambapo wanapata fursa ya kuwashirikisha na vijana wengine uzoefu wao kutoka nchini Israel. Hadi sasa jumla ya vijana 79 walioshiriki mafunzo nchini Israel ni miongoni mwa vijana 812 walio kwenye mafunzo ya kilimo biashara katika Vituo Atamizi. Baada ya kipindi cha mafunzo, watapata fursa ya kufanya kilimo biashara kupitia mashamba ya pamoja ya block farms chini ya BBT.