Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 396 2023-05-22

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa barabara ya Mangaka hadi Morogoro kupitia Mbuga ya Selous utaanza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepanga kuunganisha Mikoa ya Mtwara na Morogoro kwa barabara ya kutoka Masasi – Nachingwea – Liwale hadi Mahenge Mkoani Morogoro. Sehemu ya kutoka Masasi – Nachingwea – Liwale yenye urefu wa kilometa
175 itajengwa kwa utaratibu wa EPC + F. Kutoka Liwale – Mahenge kupitia Hifadhi ya Mbuga ya Selous Serikali imepanga kuanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika mwaka wa fedha 2023/2024. Ahsante.