Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 399 2023-05-22

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga hospitali kubwa katika Mkoa wa Kagera?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bernadetha Kasabago Mushashu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kagera una Hospitali kubwa ya Mkoa ambapo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imekamilisha jengo la huduma za dharura (EMD) ambalo limegharimu shilingi 560,000,000, jengo la uangalizi (ICU) lililogharimu shilingi 650,000,000, jengo la huduma za mionzi (Radiology) lililogharimu shilingi 237,000,000, nyumba ya mtumishi iliyogharimu shilingi 90,000,000 pamoja na ununuzi na ufungaji wa mashine ya CT-Scan ambayo imegharimu kiasi cha shilingi 1,810,000,000 na huduma zimeanza kutolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kupeleka fedha zaidi kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera ikizingatia pia kuboresha eneo la majanga na magonjwa ya mlipuko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.