Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 9 2023-08-29

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA: Aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa ya Kitulo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuitangaza hifadhi ya Taifa Kitulo Kitaifa na Kimataifa kwenye maonyesho na matamasha mbalimbali kama vile Karibu Kusini, Kili-fair, Sabasaba, na Nanenane. Pia, tumeanza kuitangaza kwa njia ya kidigitali, mitandao ya kijamii, majarida na Safari Channel. Lengo ni kuvutia watalii na wawekezaji.

Mheshimiwa Spika, aidha, Wizara imeanza kuboresha miundombinu ndani ya hifadhi ikiwemo ujenzi wa nyumba tatu na tunatarajia kujenga nyumba mbili na kambi moja ya kuweka hema katika mwaka huu wa fedha wa 2023/2024, pamoja na kukarabati miundombinu ya barabara.