Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 13 2023-08-29

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kutatua changamoto za wakulima waliowekeza kwenye SACCOS na fedha zao kupotea?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa upotevu wa fedha za wanachama wa SACCOS nchini unadhibitiwa ipasavyo, Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika inayo mikakati mbalimbali, ikiwemo kutoa miongozo ya uendeshaji na usimamizi wa Vyama vya Ushirika nchi zikiwemo SACCOS, kuanza kutumia Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (MUVU), ambao utasaidia kuongeza uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji na usimamizi wa shughuli za Vyama vya Ushirika, zikiwemo SACCOS, kuendelea kutoa elimu ya ushirika kuhusu namna bora ya uendeshaji na usimamizi wa Vyama vya Ushirika kwa wananchi wote, wakiwemo wanachama, viongozi na watendaji wa SACCOS kupitia njia mbalimbali.