Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 441 2023-05-26

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kujenga kilometa moja ya lami nyepesi Mabira Station ili kuboresha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitenga bajeti ya ujenzi na matengenezo ya barabara hiyo ambapo katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 shilingi milioni 117.14 zilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa kilometa saba za barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, shilingi milioni 83.1 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa kilometa nne kwa kiwango cha changarawe na ujenzi umekamilika. Vilevile katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, barabara ya Mabira Station imetengewa shilingi milioni 47.6 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kujenga kilometa moja ya lami nyepesi Mabira Station kulingana na upatikanaji wa fedha ili kuboresha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara.