Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 442 2023-05-26

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali iliajiri watumishi 7, 736 wa Afya na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilipangiwa watumishi 104 na watumishi saba walipangwa Hospitali ya Halmashuri ya Wilaya ya Meatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2022/2223, Serikali itaajiri watumishi wa kada ya afya 8,070. Aidha, baada ya taratibu za ajira kukamilika watumishi hao watapangwa kwenye Halmashauri zote nchini ikiwemo Halmashauri ya Meatu.