Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 443 2023-05-26

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID K.n.y. MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya uhakiki ili kuwarejesha walengwa 2,500 waliosimamishwa kupokea ruzuku ya TASAF?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kuanza utekelezaji wa Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu ya TASAF, mwaka 2019 na 2021 Serikali iliagiza kufanyika uhakiki wa walengwa wote wa TASAF ili kupata taarifa sahihi ya walengwa wote waliomo katika kanzidata. Zoezi la uhakiki lilifanyika katika maeneo yote nchini na baadhi ya kaya zilibainika kukosa vigezo vya kuwa kwenye orodha ya walengwa na hivyo kusimamishwa kupokea ruzuku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kaya ambazo zilithibitika kuwa na vigezo zimepewa nafasi ya kukata rufaa kwa mujibu wa sheria na taratibu na zilizobainika kuwa ni kweli zilikuwa na vigezo vya kuendelea kuwa kwenye mpango zilirejeshwa.