Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 444 2023-05-26

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje kukomesha uvuvi haramu wa kuvua samaki kwa kutumia nyavu zenye matundu madogo?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aleksia Asia Kamguna, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaboresha mfumo wa utoaji wa vibali vya kuingiza zana za uvuvi nchini ili kudhibiti uingizwaji wa zana haramu ikiwemo nyavu zenye matundu madogo na makokoro. Aidha, Serikali inaendelea kuimarisha shughuli za ukaguzi wa zana za uvuvi zinazoingizwa nchini kupitia njia za mipakani na bandarini kwa kuongeza idadi ya watumishi na vitendea kazi. Hili litaongeza wigo wa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maeneo ya mipakani na bandarini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Ofisi ya Rais - TAMISEMI imeandaa Mkakati wa muda mfupi na muda mrefu wa kudhiti vitendo vya uvuvi haramu nchini. Utekelezaji wa mkakati huo utashirikisha viongozi wa ngazi za Vijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na Mikoa ili kudhibiti matumizi ya zana haramu ikiwemo nyavu zenye matundu madogo, kokoro na nyinginezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali itaendelea kutoa elimu kwa wavuvi, waingizaji na wasambazaji wa zana za uvuvi pamoja na jamii kwa ujumla kuhusu athari za matumizi ya zana haramu za uvuvi zikiwemo nyavu zenye matundu madogo, kokoro, timba, freemaya pamoja na matumizi ya vilipuzi katika uvuvi, ahsante.