Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 445 2023-05-26

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, lini Serikali itatafuta suluhisho la kudumu la kudhibiti wanyama waharibifu wa mazao na ugonjwa wa mnyauko?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge Nkenge wa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Kilimo kila mwaka hutenga fedha kwa ajili ya kudhibiti makundi mbalimbali ya wanyama waharibifu wa mazao hususani panya, kweleakwelea, viwavijeshi na nzige.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2022/2023, jumla ya shilingi bilioni 4.9 zimetolewa kwa ajili ya kudhibiti wanyama hao. Aidha Serikali inaendelea kuimarisha timu ya kusimamia kilimo anga ambapo ndege moja iliyokuwa mbovu imesharekebishwa na taratibu za kununua ndege mpya zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na ugonjwa wa mnyauko katika mazao mbalimbali ikiwemo ndizi, viazi, maharage na kahawa, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuzalisha miche bora yenye ukinzani na magonjwa ya mnyauko; kutoa elimu kwa wakulima na Maafisa Ugani kuhusu kukata au kung’oa mashina yote yaliyoathirika na kuyachoma moto ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa na kuzalisha miche bora kutoka mashina yaliyoathirika kutumia teknolojia ya tissue culture ambayo inasaidia kusafisha na kuzalisha miche ambayo haitakuwa na ugonjwa huo.