Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 447 2023-05-26

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -

Je, watalii wangapi walitembelea Mbuga ya Ruaha kwa mwaka 2019/2020 na upi mkakati wa kuongeza watalii?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasilinna Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2019/2020 Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ilipokea jumla ya watalii 18,678 ambapo watalii 11,601 kutoka nje ya nchi na watalii 7,077 kutoka ndani ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha idadi ya watalii inaongezeka, Serikali imeweka mikakati ifuatayo: -

(i) Kuanzisha na kuboresha miundombinu ya barabara za ndani ya hifadhi kwa kiwango cha changarawe na kuboresha barabara kuu kutoka Iringa Mjini hadi hifadhini.

(ii) Kuongeza na kuboresha viwanja vya ndege saba ndani ya hifadhi.

(iii) Kuongeza miundombinu ya malazi kwa kuongeza vitanda 263 na kutangaza maeneo ya uwekezaji.

(iv) Kuongeza na kuboresha mazao ya utalii kama utalii wa puto, boti, farasi, kuvua samaki, utalii wa kitamaduni na kihistoria, utalii wa mikutano na utalii wa michezo.

(v) Kuongeza utangazaji wa vivutio vya hifadhi katika masoko ya ndani na nje ya nchi.