Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 448 2023-05-26

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, lini Kata za Miyombweni, Malilo, Songwe na Luhanga zitawekwa anuani za makazi?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 8 Februari, 2022 Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alielekeza utekelezaji wa mfumo wa anwani za makazi ufanyike kwa njia ya operesheni kwa usimamizi wa Wakuu wa Mikoa na kwamba utekelezaji wake ukamilike mwezi Mei, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais ulifanyika kwa tija na ufanisi mkubwa ambapo hadi Mei, 2022 Halmashauri, Kata, Vijiji, Mitaa, Shehia zote nchini zilikuwa zimefikiwa. Aidha, utekelezaji ulifanyika kwa kuzingatia miongozo iliyopo ikiwa ni pamoja na kutotoa anwani za makazi maeneo ambayo ni hatarishi yasiyoruhusiwa kwa makazi mfano, mabondeni, kwenye vyanzo vya maji, maeneo oevu, maeneo ya hifadhi, maeneo ya wazi na maeneo ya hifadhi ya barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya Kata za Miyombweni, Malilo Songwe na Luhanga zipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ahsante.