Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 449 2023-05-26

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vyuo vya VETA katika Wilaya za Liwale, Nachingwea, Ruangwa na Lindi Vijijini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kujenga Chuo cha Ufundi Stadi katika kila Mkoa na Wilaya nchini. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 100 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vyuo vya VETA katika Wilaya 64 ambazo zilikuwa hazijajengewa vyuo hivyo. Tayari Serikali imeshakamilisha kuandaa michoro na upatikanaji wa maeneo kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale na Nachingwea ni miongoni mwa Wilaya 64 ambazo zipo kwenye mpango wa kujengewa Vyuo vya Ufundi Stadi kwa mwaka huu wa fedha. Tayari kiasi cha shilingi 228,942,380 kimeshatolewa kwa kila chuo kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vyuo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Ruangwa umeshakamilika kwa gharama ya shilingi bilioni 2.3 na mafunzo yameshaanza kutolewa. Aidha, kwa Wilaya ya Lindi tayari kipo chuo cha mkoa kinachoweza kutumiwa na wananchi wa Halmashauri ya Lindi Vijijini, nakushukuru.