Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 74 2023-09-05

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:-

Je, ni mafunzo ya aina gani yanatolewa kwa vijana wa Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu inatoa mafunzo ya ujuzi Stadi na stadi za kazi kwa nguvu kazi ya vijana iliyopo katika soko la ajira, yaani kwa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu na mafunzo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mafunzo yanayotolewa ni: -

(i) Mafunzo ya kukuza ujuzi wa ufundi katika fani mbalimbali kwa njia ya Uanagenzi yaani Apprenticeship training ambapo kijana anatumia zaidi ya 60% ya muda wa mafunzo katika maeneo ya kazi;

(ii) Mafunzo ya kurasimisha ujuzi unaopatikana nje ya mfumo rasmi wa elimu na mafunzo yaani Recognition of Prior Learning Skills ambapo vijana wanafanyiwa tathmini ya mapungufu waliyonayo, kupatiwa mafunzo na hatimaye kupatiwa vyeti ambavyo vitawasaidia kuendelea na mafunzo ngazi zinazofuata kwa ajili ya kuajiriwa au kujiajiri;

(iii) Mafunzo ya Uzoefu wa Kazi kwa wahitimu yaani Internship Training ambapo wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu wanapelekwa maeneo ya kazi kujifunza kazi;

(iv) Mafunzo ya kukuza ujuzi kwa wafanyakazi waliopo makazini yaani Skills Updating and Upgrading ili kuziba mapengo ya ujuzi yanayotokana na mabadiliko ya teknolojia na utendaji wa kazi na utoaji wa huduma;

(v) Mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi wa biashara, miradi, Urasimishaji na Uendelezaji. Mafunzo haya huenda sambamba na utoaji mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana;

(vi) Mafunzo ya Stadi za Maisha kwa Vijana hasa wale walio nje ya mfumo wa shule ili kuwawezesha kujitambua, kuwa na uzalendo na kufanya maamuzi sahihi kuhusu maisha yao, ahsante.