Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 93 2023-09-06

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: -

Je, lini jengo jipya la X-Ray litajengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia fursa ya mikopo inayotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) inakamilisha taratibu za kupata mkopo wa shilingi milioni 190, kwa ajili ya ujenzi wa jengo la X–Ray katika Hospital ya Wilaya ya Maswa.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kutokana na uchakavu wa baadhi ya majengo Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024 imetenga kiasi cha shilingi milioni 900, kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa majengo katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa. Ahsante.