Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 94 2023-09-06

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga barabara za mitaa za Mkoa wa Dar es Salaam kwa mfumo wa EPC+F kwa vile Mradi wa DMDP haukidhi haja?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Massaburi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na ukamilishaji wa maandalizi ya Mradi wa DMDP Awamu ya Pili. Tayari wataalam washauri watatu wanaendelea na kazi ya usanifu ambapo mkataba wa kazi hiyo utafanyika kwa muda wa miezi sita kuanzia Tarehe 30 Mei, 2023. Mara tu usanifu utakapokamilika, taratibu za ununuzi wa kuwapata wakandarasi zitaanza kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, EPC+F ni mfumo wa ujenzi wa kimkataba ambapo mkandarasi anafanya usanifu, ununuzi, ujenzi na kugharamia kazi za ujenzi (engineering design, procurement, construction and financing). Serikali kupitia TARURA bado haijaanza kutekeleza mfumo huu. Serikali inapokea ushauri na itapitia na kuufanyia kazi.